Friday, January 25, 2013

Siku kuu ya Uongofu wa Mtume Paulo

Sikukuu ya Wongofu wa Mtume Paulo ni sikukuu inayoadhimishwa katika mwaka wa kiliturujia Januari 25, ikinukuu uongofu wake. Mbali na kanisa Katoliki, sikukuu hia pia inaadhimishwa na makanisa mbalimbali ya Mashariki Orthodox, Oriental Orthodox, Anglikana na makanisa ya Kilutheri. Kutokana na kuadhimishwa na makanisa haya mbalimbali, sikukuu hii inakua ni hitimisho la wiki ya maombi ya kuombea Umoja wa Wakristu duniani. Wiki hii ya maombi hufanyika kila mwaka kuanzia Januari 18 mpaka Januari 25


Mtakatifu Paulo alizaliwa kati ya miaka 7-10 BK katika familia ya Kiyahudi ya kabila la Benyamini (Israeli) na madhehebu ya Mafarisayo iliyoishi katika mji wa Tarsus (kwa sasa mji huo uko sehemu ya kusini mashariki ya nchi ya Uturuki).
Jina lake la kwanza (la Kiebrania) lilikuwa Sauli, lakini kadiri ya desturi ya wakati ule alikuwa pia na jina la Kigiriki: Paulos kutoka Kilatini Paulus. Mwenyewe alikuwa na uraia wa Roma kama wananchi wote wa Tarsus. Angali kijana alisomea ualimu wa Sheria (yaani wa Torati) huko Yerusalemu chini ya mwalimu maarufu Gamalieli wa madhehebu ya MafarisayoAkishika dini yake kwa msimamo mkali akawa anapinga Ukristo kwa kuwakamata, kuwatesa na hata kuwaua Wakristo, kama vile Stefano Mfiadini mpaka alipotokewa na Yesu Kristo mfufuka akiwa njiani kwenda Damaski (kwa umuhimu wake katika historia ya wokovu habari hii inasimuliwa mara tatu katika kitabu cha Matendo ya Mitume: 9:1-19; 21:12-18 na 22:5-16). Jibu lake kwa Yesu lilikuwa (Mdo 22:10): "Nifanye nini, Bwana?"

Baada ya Wongofu na baada ya kufanya utume katika mazingira ya Kiarabu, Tarsus na Antiokia alianza kufanya safari za kitume, akienda mbali zaidi na zaidi, akilenga kumhubiri Yesu mahali ambapo bado hajafahamika, hata Hispania.
Ilikuwa kawaida yake kuanzisha Kanisa katika miji mikubwa ili toka huko ujumbe ufike hadi vijijini.
Muda wote wa utume wake Paulo alipambana na dhuluma kutoka kwa Wayahudi wenzake na matatizo mengine kutoka Wakristo wenye msimamo tofauti na wa kwake hasa kuhusu haja ya kufuata masharti ya Agano la Kale ili kupata wokovu.
Hatimaye alikamatwa na wapinzani wake Wayahudi mjini Yerusalemu, lakini askari wakoloni walizuia asiuawe. Baada ya hapo alilazimika kukaa gerezani akisubiri hukumu ya Dola la Roma, kwanza Kaisaria Baharini miaka miwili, halafu akakata rufaa kwa Kaisari akapelekwa Roma, alipofika mwaka 61 akakaa miaka miwili tena kifungo cha nje katika nyumba ya kupanga.

Aliuawa nje ya kuta za Roma kwa kukatwa kichwa wakati wa dhuluma za Nero kati ya mwaka 64 na 67 B.K. Kati ya barua nyingi alizoandikwa kwa makanisa ya Thesalonike, Korintho, Galatia, Roma, Filipi, Kolosai,Efeso, kwa viongozi Wakristo kama Timotheo na Tito, tena kwa Filemoni, katika Agano Jipya zinatunzwa 13. Ukubwa na ubora wa mchango wa Paulo unaeleweka tukizingatia kwamba alifanya kazi na kuandika kabla ya vitabu vya Agano Jipya kupatikana. Ndiye aliyeanza kuliandika akipanua mawazo aliyoyapokea katika Kanisa kwa kuzingatia Agano la Kale na mang’amuzi yake mwenyewe.










1 comment:

  1. Mr Green Casino - Dr.MCD
    Mr Green 안성 출장마사지 Casino is an international game 속초 출장샵 provider and provider of online entertainment. Get the latest 전라남도 출장마사지 casino news, insights and updates. Rating: 4.1 인천광역 출장안마 · ‎14 reviews 남원 출장마사지

    ReplyDelete