Tuesday, January 8, 2013

Epifania - Siku kuu ya Toleo la Bwana

Kila tarehe 6 Januari,  Kanisa linasheherekea   Siku kuu ya "Toleo la Bwana" inayotambulika kama Epifania. Hii ni Sherehe ambayo Mfalme Masiha anajitambulisha wazi katika Ulimwengu. Injili ya Mathayo 2:1-2 inazungumzia Mamajuzi waliofuata mwongozo wa nyota ili wakamwone Masiha na kumsujudia. Ni kwa njia ya nyota, Mamajusi wanaweza kufika mahali alipokuwa na wakaweza kumsujudia na kumpatia zawadi zao. Kumbe Yesu Kristo Masiha ni nyota inayaangaza na kuongoza maisha yetu mpaka mwisho wa nyakati hadi kufika mbinguni. Katika Siku kuu ya Krismasi tarehe 25 Disemba, Kristo anajitoa katika watu ulimwenguni. Siku kuu ya Toleo la Bwana yaani "Epifania" Mamajusi wanawakilisha watu wote ulimwenguni wanaojitolea kwa Bwana kwa kumwabudu, kumwamini na kumsujudia

No comments:

Post a Comment